Saturday, October 12, 2013

Zitto na tuhuma nzito kwa wabunge wa CCM kuhujumu Katiba


Zitto Kabwe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe amesema kuna njama inayofanywa na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutaka mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya usiishe ili wajiongezee muda hadi mwaka 2017.

Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema kuwa lengo la wabunge hao ni kutaka muda wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 usogezwe mbele hadi 2017 ili waendelee kukaa madarakani.
Alisema kuwa CHADEMA haitakubali uvunjwaji wa aina yoyote wa katiba, na hivyo kumtahadharisha Rais Jakaya 
Kikwete kutothubutu kukubaliana na fitna hizo.



Madai ya Zitto yaliwahi pia kutolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alisema kuwa CCM wanataka kukwamisha mchakato wa katiba makusudi ili kutengeneza sababu ya kuongeza muda wa Rais Kikwete kubaki madarakani kwa miaka miwili zaidi.

Prof. Lipumba alisema kuwa hoja ambayo CCM wanataka kuitumia kukwamisha mchakato huo, ni muundo wa serikali ambapo dakika za mwisho wanataka kukubali serikali tatu kisha watumie kisingizio cha uundwaji wa taifa la Tanganyika kuchelewesha katiba mpya.

Akihutubia mikutano mbalimbali ya hadhara katika Jimbo la Bukene mkoani hapa, ukiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya ujenzi wa chama katika Kanda ya Magharibi jana, Zitto alisema hata vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni na Naibu Spika Job Ndugai, kuruhusu askari waingie ndani ya Bunge kuwakamata na kuwapiga wabunge wa upinzani, ilikuwa ni sehemu ya mpango huo wa kutaka kusogezwa mbele kwa muda wa wabunge kutoka madarakani.

Zitto alifafanua kuwa hoja inayojengwa na wabunge hao ambao wameshaanza kuipenyeza kwa ajili ya kumfikia Rais Kikwete, ni kwamba kama katiba mpya itapatikana kwa wakati huu, muda wa kujiandaa na uchaguzi wa mwaka 2015 utakuwa hautoshi.
“Hawa ni wabunge waroho wa madaraka, hawajafanya jambo lolote jema katika majimbo yao, na sasa wanajua hawawezi kurudi ndiyo maana wanataka muda usogezwe na wao waendelee kulipwa mshahara na posho.
“Sisi CHADEMA tunasema hilo hapana, hatuwezi kukubali uchaguzi usogezwe kwa miaka miwili, na namuonya Rais 

Kikwete asithubutu kuingia katika mkenge huo unaowahusisha baadhi ya mawaziri,” alisema.
Aliongeza kuwa wananchi waliwachagua wabunge wao kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano, na kwamba kuwe na katiba mpya au isiwepo ni muhimu uchaguzi kufanyika ili wale walioshindwa kuwajibika wakae pembeni.

Zitto alisema CHADEMA inatoa kauli hiyo ili wananchi wajue mkakati huo, na washiriki kuupigia kelele, kwa kile alichoeleza kuwa mipango hiyo imeshaanza jijini Dar es Salaam na Dodoma.

Kwa mujibu wa Zitto, baadhi ya mawaziri wanataka kutumia nafasi ya kuwa karibu na rais ili kumshawishi akubali mkakati huo, kwa kumueleza kuwa hali hiyo itamjengea heshima na kumbukumbu ya kuiachia nchi katiba iliyo bora.

Avunja ngome ya CCM
Katika hatua nyingine, Zitto ameitikisa ngome ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi.
Dalili ya ngome hiyo kutikiswa ilianza kuonekana mapema wiki hii wakati viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Uyui walipokuwa wakifanya maandalizi ya mkutano katika Kata ya Mabama, ambako ni nyumbani kwa kigogo huyo.

Baada ya kutangazwa kuwapo kwa mkutano wa CHADEMA katika kata hiyo, gazeti hili lilishuhudia jitihada mbalimbali za viongozi wa CCM zikifanyika, ikiwemo kuweka bendera mpya kila baada ya nyumba mbili, huku zile nyumba za wakazi wasiokuwa wafuasi wa chama hicho, zikiwekwa barabarani.

Baadhi ya wakazi wa kata hiyo na maeneo mengine ya jirani ambao walijitokeza kumsikiliza Zitto, walieleza kuwa baadhi ya nyumba zilizowekwa bendera wakazi wake walitishiwa kufanyiwa hujuma kupitia ofisi ya mtendaji wa kata hiyo endapo wangekataa.
“Unaona bendera zote ni mpya, hapa tumewachoka, na sasa wanatumia vitisho kutaka kuweka bendera zao kwenye nyumba zetu,” alisema mmoja wa wakazi hao ambaye hakutaka kutajwa jina.

Hata hivyo, mkutano wa Zitto nusura uingie dosari baada ya msafara wake kuchelewa kufika katika Kata ya Mabama, kisha mtu aliyejitambulisha kama ofisa mtendaji wa kata hiyo, kuwataka wananchi watawanyike kutoka katika uwanja wa mkutano.

Lakini wananchi hao hawakukubaliana na agizo hilo na kuahidi kumsubiri Zitto ambaye aliwasili katika eneo la mkutano saa 12:47 jioni na kuwahutubia hadi saa moja na robo usiku.

Kabla ya kuhutubia mkutano huo, Zitto aligawa kadi kwa wanachama wapya waliotoka CCM na kuwataka wasiogope vitisho vyovyote vinavyofanywa na viongozi wa chama hicho.
Alisema CCM imeua njia ya reli iliyokuwa ikiwasaidia wakazi wa Mabama kufanya shughuli za kila siku za kujipatia kipato.

Hata hivyo, Wakasuvi alikanusha chama chake kujihusisha na vitendo vya kuwatisha wananchi, akisema kuwa wao wanatumia nguvu ya hoja.

4 comments:

oakleyses said...

burberry outlet, nike outlet, oakley sunglasses, kate spade outlet, michael kors outlet online, tiffany and co, tiffany jewelry, michael kors outlet online, louis vuitton, christian louboutin, michael kors outlet, louis vuitton outlet, nike air max, ray ban sunglasses, louis vuitton, cheap oakley sunglasses, michael kors outlet online, gucci handbags, prada handbags, michael kors outlet, uggs on sale, longchamp outlet, tory burch outlet, ray ban sunglasses, christian louboutin shoes, uggs outlet, oakley sunglasses, christian louboutin uk, ray ban sunglasses, longchamp outlet, chanel handbags, nike free, ugg boots, uggs outlet, prada outlet, louis vuitton outlet, replica watches, oakley sunglasses wholesale, christian louboutin outlet, polo ralph lauren outlet online, jordan shoes, burberry handbags, nike air max, replica watches, ugg boots, oakley sunglasses, polo outlet, longchamp outlet

oakleyses said...

lululemon canada, ray ban pas cher, michael kors pas cher, burberry pas cher, sac vanessa bruno, north face, nike air force, hollister uk, coach outlet, abercrombie and fitch uk, nike air max uk, nike blazer pas cher, nike air max uk, new balance, coach outlet store online, nike roshe, true religion outlet, sac longchamp pas cher, timberland pas cher, true religion jeans, polo ralph lauren, mulberry uk, coach purses, true religion outlet, guess pas cher, nike tn, nike free run, sac hermes, michael kors, ray ban uk, hollister pas cher, north face uk, ralph lauren uk, nike air max, polo lacoste, converse pas cher, oakley pas cher, air max, replica handbags, true religion outlet, michael kors, kate spade, vans pas cher, michael kors outlet, louboutin pas cher, nike roshe run uk, hogan outlet, longchamp pas cher, jordan pas cher, nike free uk

oakleyses said...

moncler, ugg uk, replica watches, moncler, louis vuitton, canada goose outlet, lancel, louis vuitton, karen millen uk, doudoune moncler, pandora charms, links of london, canada goose outlet, juicy couture outlet, moncler, vans, juicy couture outlet, ray ban, coach outlet, thomas sabo, converse, moncler outlet, marc jacobs, hollister, moncler uk, pandora jewelry, canada goose outlet, barbour uk, ugg pas cher, hollister, nike air max, canada goose jackets, swarovski, louis vuitton, ugg, pandora jewelry, converse outlet, swarovski crystal, wedding dresses, canada goose, canada goose, louis vuitton, moncler, ugg,uggs,uggs canada, barbour, canada goose, louis vuitton, toms shoes, moncler outlet, ugg,ugg australia,ugg italia, gucci, pandora uk, supra shoes

oakleyses said...

nike air max, longchamp outlet, louis vuitton, nike outlet, prada handbags, ray ban sunglasses, jordan shoes, ugg boots, tiffany and co, ray ban sunglasses, polo outlet, nike free, christian louboutin outlet, louis vuitton, prada outlet, chanel handbags, ray ban sunglasses, christian louboutin uk, nike air max, longchamp outlet, louis vuitton outlet, tiffany jewelry, kate spade outlet, uggs on sale, oakley sunglasses, louis vuitton outlet, christian louboutin shoes, longchamp outlet, polo ralph lauren outlet online, gucci handbags, replica watches, replica watches, tory burch outlet, oakley sunglasses wholesale, ugg boots, oakley sunglasses, cheap oakley sunglasses, oakley sunglasses, christian louboutin, louis vuitton outlet