Saturday, June 15, 2013
Friday, June 14, 2013
Wengi wameikosoa bajeti walalahoi kulia
| Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa |
Kwa tafsiri yoyote ile, bajeti hiyo inaonyesha bayana kwamba sio endelevu, kwani kati ya fedha hizo, Sh12,575 trilioni zitakuwa za matumizi ya kawaida wakati Sh5,674 trilioni tu ndizo zitatumika katika miradi ya maendeleo.
Thursday, June 13, 2013
CCM haitaki serikali tatu na mgombea binafsi
Chama hicho tawala kimesema bado kinaamini katika muundo wa Serikali mbili.
Kuhusu mgombea binafsi pamoja na kwamba hajafafanua kwa undani lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaeleza ndio msimamo wa chama hicho kwa vile serikali ya chama hicho imekuwa ikipinga suala hilo kwa muda mrefu.
Tuesday, June 11, 2013
Monday, June 10, 2013
CHADEMA, CUF waunga mkono serikali taatu
![]() |
| Pro. Ibrahim Lipumba |
![]() |
| Freeman Mbowe |
Mbowe Amesema mambo mengi yaliyopendekezwa na chama chake yamefanyiwa kazi na Tume ya Mabadiliko na kuishangaa CCM akidai kwamba inapinga rasimu hiyo hususan suala la Serikali tatu wakati kimsingi watu wa Tanzania Bara wamekuwa wakipunjika kwenye muundo wa sasa wa Muungano.
Sunday, June 9, 2013
Taifa Star yafungwa na Morocco 2 - 1 , Ivory Coast yaibanjua Gambia 3 - 0
Tanzania ambayo ilionyesha udhaifu mkubwa katika kiungo na ushambuliaji ilistahili kichapo hicho kwani kwa wale wanaofahamu soka watukubaliana kuwa ilistahili kupata adhabu hiyo kwa vile Morocco walitawala mchezo huo kuanzia kipindi cha kwanza hadi cha pili.
Goli pekee la Taifa Stars lilifungwa na Amri Kiemba kwa shuti kali kutoka umbali wa mita kama 40.
Kwa matokeo hayo Tanzania inabakia nafasi ya pili na pointi 6 huku Ivory Coast wakiendelea kuongoza kundi C kwa kuwa na point 10 baada ya jana pia kuifunga Gambia jumla ya magoli 3 - 0.
Taifa Stars wanahitaji kushinda mechi baina yake na Ivory Coast siku ya jumapili ijao katika uwanja wa Taifa ili kupunguza tofauti ya pointi. Mechi kati Ivory Coast na Stars itachezwa Jumapili hapa nyumbani kuanzia saa 9 alasiri.
Msimamo kamili wa kundi C baada ya mechi za jana huu hapa chini
KUNDI C
| Team | MP | W | D | L | GF | GA | Pts |
|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Ivory Coast | 4 | 3 | 1 | 0 | 10 | 2 | 10 |
Tanzania | 4 | 2 | 0 | 2 | 6 | 6 | 6 |
Morocco | 4 | 1 | 2 | 1 | 6 | 7 | 5 |
Gambia | 4 | 0 | 1 | 3 | 2 | 9 | 1 |
Saturday, June 8, 2013
Mauaji ya kutisha Sengerema
| Mbunge wa Sengerema William Ngeleja |
Hofu kubwa na simanzi imewakumba wakazi wa mji wa Sengerema akiwemo Mbunge wa jimbo hilo, William Ngeleja, baada ya Jeshi la Polisi wilayani humo kwa kushirikiana na wananchi kugundua makaburi mawili yaliyozikwa watu wawili wakiwa wamejeruhiwa vibaya na kuvunjwa shingo.
Miili ya watu hao ilipatikana ikiwa imefukiwa katika makaburi mawili tofauti yenye urefu wa kina cha futi mbili ikiwa imeharibika vibaya, katika kitongoji cha Mnadani kata ya Nyampurukano na kusababisha watu walioshuhudia kuangua kilio na wengine kuzirai.
Tuesday, June 4, 2013
Katiba mpya moto, muundo wa serikali tatu yawashtua wengi
Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.
Mabadiliko mengine yaliyosheheni kwenye rasimu hiyo ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge, suala la maadili ya viongozi wa taifa, umri wa urais kubaki kama ulivyokuwa na kuruhusiwa kwa wagombea binafsi katika ngazi zote; urais, ubunge, udiwani mpaka ngazi za mitaa.
Monday, June 3, 2013
Katiba Mpya yakamilika kuandikwa, rasimu kuzinduliwa leo
![]() |
Mwelekeo wa Taifa la Tanzania utaanza kujulikana leo mchana Tume ya Mabadiliko ya Katiba itakapozindua rasimu ya Katiba Mpya kwenye tukio la kihistoria litakalofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.
Watanzania wanasubiri kwa hamu kuona kama rasimu hiyo itakuja na majibu ya maswali magumu, makubwa ya muundo wa Muungano, madaraka ya Rais, uteuzi wa mawaziri kutokana na wabunge, muundo wa wakuu wa mikoa/wilaya na muundo wa mihimili mingine miwili ya dola; Mahakama na Bunge.
Sunday, June 2, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)








