Saturday, June 15, 2013

Bomu lalipuka mkutano wa Kampeni za CHADEMA Arusha




Baadhi ya watu waliojeruhiwa katika mlipuka huo
Hofu imetanda katika mji wa Arusha baada ya bomu kulipuka katika mkutano wa kampeni za udiwani za Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Hadi sasa habari ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa watu wawili wamefarika na mamia kujeruhiwa

Friday, June 14, 2013

Wengi wameikosoa bajeti walalahoi kulia


Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa
Serikali jana iliwasilisha Bungeni mapendekezo yake kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2013/14. Katika mapendekezo hayo, Serikali imepanga kutumia Sh18,248,983 trilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na ya maendeleo. 

Kwa tafsiri yoyote ile, bajeti hiyo inaonyesha bayana kwamba sio endelevu, kwani kati ya fedha hizo, Sh12,575 trilioni zitakuwa za matumizi ya kawaida wakati Sh5,674 trilioni tu ndizo zitatumika katika miradi ya maendeleo.

Thursday, June 13, 2013

CCM haitaki serikali tatu na mgombea binafsi


Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimepinga muundo wa Muungano wa Serikali tatu pamoja na mgombea binafsi kama ilivyopendekezwa katika rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba mwanzoni mwa wiki iliyopita.
Chama hicho tawala kimesema bado kinaamini katika muundo wa Serikali mbili.


Kuhusu mgombea binafsi pamoja na kwamba hajafafanua kwa undani lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaeleza ndio msimamo wa chama hicho kwa vile serikali ya chama hicho imekuwa ikipinga suala hilo kwa muda mrefu.

Tuesday, June 11, 2013

Unajua nini kinachomvutia Obama kuja Tanzania?

Rais wa Marekani Barak Obama 

Marekani imetaja sababu nne ambazo zimemfanya Rais Barrack Obama kuijumuisha Tanzania katika ziara yake ya bara la Afrika.
Rais Obama amepanga kulitembelea bara la Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, mwaka huu na atazitembelea pia Senegal na Afrika Kusini.

Monday, June 10, 2013

CHADEMA, CUF waunga mkono serikali taatu


Pro. Ibrahim Lipumba

Freeman Mbowe
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekiti CUF Profesa Ibrahimu Lipumba kwa nyakati tofauti wameweka bayana kuwa wanaunga mkono Rasimu ya Katiba na hasa suala la Muungano wa Tanzania kuundwa na Serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Mbowe Amesema mambo mengi yaliyopendekezwa na chama chake yamefanyiwa kazi na Tume ya Mabadiliko na kuishangaa CCM akidai kwamba inapinga rasimu hiyo hususan suala la Serikali tatu wakati kimsingi watu wa Tanzania Bara wamekuwa wakipunjika kwenye muundo wa sasa wa Muungano.

Sunday, June 9, 2013

Taifa Star yafungwa na Morocco 2 - 1 , Ivory Coast yaibanjua Gambia 3 - 0


Timu ya Taifa ya Tanzania inahitaji maajabu ili iweze kwenda Brazil kucheza kombe la dunia baada ya jana kufungwa na Morocco jumla ya magoli 2 - 1.

Tanzania ambayo ilionyesha udhaifu mkubwa katika kiungo na ushambuliaji ilistahili kichapo hicho kwani kwa wale wanaofahamu soka watukubaliana kuwa ilistahili kupata adhabu hiyo kwa vile Morocco walitawala mchezo huo kuanzia kipindi cha kwanza hadi cha pili.

Goli pekee la Taifa Stars lilifungwa na Amri Kiemba kwa shuti kali kutoka umbali wa mita kama 40.

Kwa matokeo hayo Tanzania inabakia nafasi ya pili na pointi 6 huku Ivory Coast wakiendelea kuongoza kundi C kwa kuwa na point 10 baada ya jana pia kuifunga Gambia jumla ya magoli 3 - 0.

Taifa Stars wanahitaji kushinda mechi baina yake na Ivory Coast siku ya  jumapili ijao katika uwanja wa Taifa ili kupunguza tofauti ya pointi. Mechi kati Ivory Coast na Stars itachezwa Jumapili hapa nyumbani kuanzia saa 9 alasiri.

 Msimamo kamili wa kundi C baada ya mechi za jana huu hapa chini

KUNDI C

TeamMP W D GF GA Pts
Ivory Coast431010210

Tanzania
4202666

Morocco
4121675

Gambia
4013291

Saturday, June 8, 2013

Mauaji ya kutisha Sengerema

Mbunge wa Sengerema William Ngeleja

Hofu kubwa na simanzi imewakumba wakazi wa mji wa Sengerema akiwemo Mbunge wa jimbo hilo, William Ngeleja, baada ya Jeshi la Polisi wilayani humo kwa kushirikiana na wananchi kugundua makaburi mawili  yaliyozikwa watu wawili wakiwa wamejeruhiwa vibaya na kuvunjwa shingo.

Miili ya watu hao ilipatikana ikiwa imefukiwa katika makaburi mawili tofauti yenye urefu wa kina cha futi mbili ikiwa imeharibika vibaya, katika kitongoji cha Mnadani kata ya Nyampurukano na kusababisha watu walioshuhudia kuangua kilio na wengine kuzirai.


Tuesday, June 4, 2013

Katiba mpya moto, muundo wa serikali tatu yawashtua wengi


Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana ilizindua rasimu ya Katiba Mpya inayopendekeza kuwapo kwa mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa utawala, yakiwamo ya kuwa na Serikali Tatu; Shirikisho la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar.
Mabadiliko mengine yaliyosheheni kwenye rasimu hiyo ni kufutwa kwa viti maalumu vya ubunge, suala la maadili ya viongozi wa taifa, umri wa urais kubaki kama ulivyokuwa na kuruhusiwa kwa wagombea binafsi katika ngazi zote; urais, ubunge, udiwani mpaka ngazi za mitaa.

Monday, June 3, 2013

Katiba Mpya yakamilika kuandikwa, rasimu kuzinduliwa leo


Mwelekeo wa Taifa la Tanzania utaanza kujulikana leo mchana Tume ya Mabadiliko ya Katiba itakapozindua rasimu ya Katiba Mpya kwenye tukio la kihistoria litakalofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam.
Watanzania wanasubiri kwa hamu kuona kama rasimu hiyo itakuja na majibu ya maswali magumu, makubwa ya muundo wa Muungano, madaraka ya Rais, uteuzi wa mawaziri kutokana na wabunge, muundo wa wakuu wa mikoa/wilaya na muundo wa mihimili mingine miwili ya dola; Mahakama na Bunge.

Sunday, June 2, 2013

Mwili wa Mangwea kuwasili jumatatu, mazishi jumanne


Mwili wa mwanamuziki wa kizazi kipya bongo fleva Marehemu Albert Mangwea utawasili kesho jumatatu kutoka Afrika ya kusini na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika siku ya jumanne nyumbani kwao Kihonda Morogoro.